WEKEZENI KWENYE VIWANDA UMEME BORA, WA UHAKIKA UPO-MHANDISI MANDA.
Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limewahimiza
wananchi kuwekeza kwenye viwanda kwakuwa hivi sasa umeme bora na wa uhakika upo.
Wito huo umetolewa leo Januari 9, 2019 Jijini
Dar es Salaam na Meneja Miradi wa Shirika hilo, anayeshughulikia uzalishaji
(Generation) Mhandisi Stephene Manda.
“Mradi wa Kinyerezi namba II wa Megawati 240 umekamilika, kwa hiyo
ombi letu kwa wote ambao wanaweza kuwekeza kwenye viwanda wawekeze kwani umeme
wa uhakika na wa kutosha upo.” Alisema.
“Itakapofika Agosti 2019 jumla ya
umeme utakaokuwa unatoka Kinyerezi pekee ni Megawati 575 kwa hivyo ni umeme wa
kutosha upo.
“Kama ni kulisha Jiji la Dar es Salaam,
basi Kinayerezi inaweza kutosha na kwa kupata umeme wa uhakika.” Alisema.
MUONEKANO wa kituo cha kufua umeme wa gesi Kinyerezi II cha Jijini Dar es Salaam,
kama kinavyoonekana katika picha ya dron iliyopigwa mwishoni mwa
Desemba 2018. Kwa mujibu wa Meneja Miradi (Uzalishaji) wa Shirika la
Umeme Nchini, (TANESCO), Mhandisi Stephene Manda, kituo hicho chenye
uwezo wa kuzalisha Megawati 240 kimekamilika.
Meneja huyo aliwahakikishia wenye
viwanda kuwa uwezo wa kuwahudumia upon a kwamba TANESCO imejipanga vizuri na
kuwaomba wawekezaji wawekeze.
Alisema hakuna ulazima kwa wawekezaji
kuwa na viwanda vikubwa, bali hata kwa vile vidogo kama vile vya kukoboa na
kusaga nafaka na vile vya kukamua matunda vitahudumiwa.
Manda alitoa wito kwa Watanzania kuuunga mkono juhudi za
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wake Rais Dk. John Magufuli, kujenga uchumi wa kati na wa viwanda
kwani inawezekana kwa vile umeme wa uhakika upo na ni bora zaidi.
No comments