MKOPO WA MASHARTI NAFUU KUMALIZA TATIZO SUGU NCHINI.
SERIKALI ya Tanzania leo J’4 March 5, 2019 imesaini mikataba
miwili ya mikopo na Benki ya Maendeleo Afrika yenye thamani ya shilingi za
kitanzania Bilioni 589.26 kwaajili ya ujenzi wa barabara inayo sababisha adha
ya usafiri kwa kipindi kirefu ya Kabingo-Kasulu-Manyovu Kigoma, yenye urefu wa kilomita
260 kwa kiwango cha lami .
Zoezi hilo limefanyika leo Jijini Dar es salaam na Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Doto James akiwakilisha Serikali ya Tanzania na
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika Alex Mubiru na kushuhudiwa na
maafisa wa Serikali pamoja na wadau mbalimbali wa Maendeleo Afrika.
Akizungumza katika hafla hiyo Doto ameishukuru Benki ya maendeleo
Afrika kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za uwekezaji katika
miundombinu ya Usafiri kwa kuwapa mikopo wa Masharti nafuu zaidi.
“Mradi huu ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya awamu ya tano
ambao unalenga uimarishaji wa miundombinu ya usafiri ili kuchochea kasi ya maendeleo
ya kiuchumi na kijamii, kupunguza umasikini na kuimarisha ushirikiano wa
Kikanda.” Amesema Doto
Ameeleza kuwa Barabara hiyo ni kiunganishi muhimu katika maendeleo na uboreshaji wa biashara
ndani na nje ya nchi hivyo utakwenda sambamba na ujenzi wa Barabara ya
Rumonge-Gitaza (km45) nchini Burundi ili kuboresha mtandao wa barabara za
Afrika Mashariki.
“Barabara hii itakapokamilika itaunganisha Bandari ya Dar es
salaam na Mikoa ya Magharibi mwa Tanzania na kufungua Masoko ya kikanda nchini Burundi,
Rwanda, Uganda na Jmhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.” Amesema Doto.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkazi wa Benki ya Maendeleo
Afrika Alex Mubiru ameipongeza Tanzania kwa jitihada zake za kuchochea kasi ya
maendeleo kiuchumi hivyo wao kama wadau wa maendeleo wapo tayari kuunga mkono
Jitihada hizo.
“Kwa niaba ya Benki ya maendeleo Afrika napenda kuthibitisha
ahadi yetu ya kuwasaidia watu naSerikali ya Tanzania katika jitihada zao za
kutambua matarajio yao kuwa Nchi ya Uchumi wa kati hivi karibuni.” Amesema Mubiru.
No comments