SURUA TISHIO LA AFYA ZA WENGI DUNIANI.
Mtaalamu wa chanjo toka Shirika la Afya Duniani
(WHO) Dkt William Mwengee
Na. Melkiory Gowelle.
Imeelezwa kuwa dhana ya kudharau
chanjo imesababisha kurejea kwa baadhi ya magonjwa ikiwemo Surua ambayo kwasasa
imekuwa tishio kwa afya za watu wengi ulimwenguni ambapo barani Afrika asilimia
700% ya watu wanaathiriwa na ugonjwa huo.
Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es
salaam na mtaalamu wa chanjo toka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt William
Mwengee, amesema nchi ya Ukrain ni kinara kwa maambukizi Duniani wakati Afrika
Taifa la Demokrasia ya Kongo linashika namba moja kwa mlipuko wa ugonjwa huo.
Kuhusu Tanzania Mwengee amesema nchi
hiyo imepiga hatua katika kutokomeza ugonjwa wa Surua, hivyo Wananchi wake hawatakiwi
kujisahau sababu chanjo ni muhimu, waendelee kuithamini ili kuboresha afya zao
juu ya magonjwa ya mlipuko.
"Surua imerudi kwa kasi sana
ambapo imeanza kuleta athari kubwa tokea mwaka jana lakini Tanzania imekuwa ni
moja kati ya nchi chache zilizo katika kiwango cha chini cha maambukizi ya
Surua na Lubela ambapo kwa mwaka jana kuliripotiwa watu 74 tu walioambukizwa.”amesema
Mwengee.
Aidha Mwengee amewataka Wanahabari
kutumia taaluma yao kuwasisitiza watanzania kuthamini na kuhudhuria chanjo za
Magonjwa yote.
“Lazima tusisitizane ili tuchanje,
kama nchi kubwa duniani zimeathiriwa vipi sisi Tanzania.? Hatutakiwi kulala
kwani tukifanya hivyo tutaumia sana.” Amesisitiza Mwangee.
Kwa upnde wake Meneja Mpango wa Taifa
wa Chanjo toka Wizara ya Afya Dr. Dafrossa Lyimo ameelezea dhamira ya Chanjo
kuwa ni kupunguza vifo ambapo kila dose moja inapunguza vifo millioni 10.6,
hivyo ni muhimu kwa atakaye anza Chanjo kufuatilia ratiba kama aina ya chanjo
hiyo inavyotaka.
“Ni muhimu sana kukamilisha ratiba ya
chanjo ili kuepuka kurudi wodini kutibiwa kutokana na kupata magonjwa hasa ya
mlipuko.” Ameeleza Dr Lyimo.
Amesema kwa sasa Wizara kupitia Idara
ya Chanjo nchini inatoa jumla ya Chanjo
tisa zinazokinga magonjwa 13 na dhamira
kuu ya idara hiyo ni kumfikia kila anayestahili kupata chanjo mahali popote kwa
usawa.
Meneja Mpango wa Taifa wa Chanjo toka Wizara ya Afya Dr. Dafrossa Lyimo
Katika hatua nyingine Mtaalamu wa
Chanjo kutoka idara hiyo Dkt. Lotalis Gadau ameelezea kuhusiana na tatizo kubwa
linalo wasumbua akina mama la Saratani ya mlango wa kizazi ambapo Wanawake elfu
50, wanapatwa na tatizo hilo kila mwaka.
Amesema ni idadi inayotishia amani na
ametaja sababu kubwa ya kufikia idadi hiyo ni dhana potofu inayoenezwa na Watu
wengi kuwa Chanjo ya HPV inayokinga Saratani hiyo inazuia akina mama kupata
ujauzito.
“Saratani hii ndio Saratani pekee
inayoongoza kwa madhara makubwa na chanjo yake inatolewa kwa mabinti wa miaka
14, hivyo waachane na uvumi, waende kwenye vituo vya afya kupata chanjo ili
kuepuka madhara.” Amesisitiza Gadau.
Idara ya Chanjo kwasasa inaadhimisha
wiki ya chanjo iliyoanza tarehe 22 mwezi huu na kumalizika tarehe 30 ambapo
inatekeleza mikakati mingi ya kupunguza vifo ili kufikia malengo yake.
No comments