Breaking News

MAABARA YA KISASA YA TAEC KUGHARIMU ZAIDI YA BILION 10.


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) Profesa Lazaro Busagala akibadilishana mktaba wa muendelezo wa ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa maabara ya TAEC, ujenzi wenye thamani ya shilingi Bilioni  10,447,749,433.24 na  Mkurugenzi  wa Kampuni ya M/S LI JUN DEVELOPMENT COMPANY LTD. maabara hiyo itajengwa kwenye makao makuu ya TAEC yaliyopo Njiro  jijini Arusha


TUME ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) September 10, 2019 imesaini mkataba wa shilingi bilioni 10,447,749,423.24 na kampuni ya ujenzi ya  M/S LI JUN DEVELOPMENT CONSTRUCTION LTD kwa ajili ya ujenzi wa awamu ya pili maabara ya kisasa.

 
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) Profesa Lazaro Busagala ameitaka kampuni hiyo kuhakikisha inajenga maabara hiyo kwa kiwango cha hali ya juu kulingana na makubaliano ya mkataba husika.

Maabara hiyo ni mwendelezo wa maabara ya awamu ya kwanza iliyozinduliwa mwezi April  mwaka huu na Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa.


Ujenzi huu wa maabara ni  juhudi zingine za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli katika kuendelea kuleta maendeleo nchini.



No comments