ESRF, UNICEF WAKUTANA NA SERIKALINI KUPATA UFUMBUZI WA CHANGAMOTO ZA WATOTO NA VIJANA MAENEO YA MIJINI.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria warsha hiyo wakiwa katika picha
ya pamoja baada ya kumalizika kwa warsha hiyo ya kujadili namna ya kutatua
changamoto za watoto mtoto na vijana katika majiji na miji, warsha iliyofanyika
jijini Dodoma tarehe 11 Septemba 2019.
Na Ezekiel Mtonyole, Dodoma.
KATIKA kuhakikisha
changamoto za watoto na vijana maeneo ya Mijni zinapatiwa ufumbuzi, jana tarehe
11 Septemba 2019 Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) kwa
kushirikiana na UNCEF, kupitia Maabara ya Ukuaji wa Miji Tanzania (TULab),
wamewakutanisha wadau na wataalam kutoka serikalini kujadiliana namna ya
kumlinda mtoto hasa maeneo ya mijini.
Akizungumza wakati wa
Warsha hiyo Mkuu wa Idara ya Utafiti Mkakati na Machapisho kutoka ESRF,
Profesa Fortunata Makene, amesema lengo la kukutana kwa wadau hao ni
kupata maoni yatakayosaidia kuanzisha programu itakayosaidia kutatua changamoto
za watoto na vijana ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mtoto analindwa.
Kwa kuweka mazingira
mazuri katika majiji na miji.
Amesema warsha kama hii
iliofanyika Dodoma itafanyika pia Mikoa ya Dar es saalam na Mbeya, ambapo
watakutana na wadau kutoka Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali (NGO’s), Sekta
Binafsi pamoja na watoto wenyewe.
Amesema washiriki wa
warsha ya leo ni wataalam zaidi ya 20 kutoka serikalini yaani TAMISEMI,
Ofisi ya Takwimu, Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto,
Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma, Chuo
Kikuu cha Dodoma nk., wote hawa wakiwa ni wadau wa ukuaji wa miji.
Ilielezwa katika kupanga
miji ni lazima mipango hiyo iwe rafiki kwa watoto ili isiweze kuwaathiri,
amesema watoto wamekuwa wakiathiriwa sana na ukuaji wa miji na hata wengine
kujiingiza katika mambo ambayo yanawaathiri na kushindwa kufikia malengo yao.
Miongoni mwa changamoto
zilizotajwa katika miji ambazo zimekuwa zikiwaathiri au kuathiri ukuaji
kwa watoto ni pamoja na ajira za watoto, hii imetajwa kuwa ni changamoto ambayo
imekuwa ikiathiri watoto kwa sababu watoto wengi wamekuwa wakijiingiza katika
kutafuta kipato kujikimu.
Upatikanaji wa maji hasa
kwa maeneo ambayo hayajapimwa imekuwa ni changamoto kwa sababu watoto ndio
huenda kutafuta maji na huko ndio hukutana na vitendo ambavyo huwaathiri katika
ukuaji wao kwa matukio ya ukatili.
Mitandao ya kijamii pia
imetajwa kama ndio chanzo cha watoto wa mijini kuathiriwa katika ukuaji wao
tofauti na watoto wa vijijini, pia wadau wameshauri kuendelea kutoa elimu
kwa watoto ili waepukane na athari hizo.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Watoto kutoka wizara ya Afya Maendeleo ya
Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Mwajuma Magwiza, amesema serikali imekuwa
ikifanya jitihada mbalimbali ikiwamo kuanzisha dawati la watoto.
Pia uanzishwaji wa huduma
ya simu kwa watoto kupitia namba 116, ambayo mpaka sasa imesaidia kusikilizwa
kwa mashauri 43 ya watoto yakijumuisha ubakaji, mimba na ndoa za utotoni, Pia
wamefanikiwa kutoa huduma muhimu kwa watoto 329 wanaoishi kwenye vituo vya
kulelea watoto.
Mgeni rasmi katika warsha
hii alikuwa Dr. John K. Jingu, Katibu Mkuu, Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii
Jinsia Wazee na Watoto, ambaye aliwakilishwa na Mwajuma Magwiza, Mkurugenzi,
Maendeleo ya watoto.
No comments