Breaking News

WATANZANIA WATAKIWA KUPINGA RUSHWA YA NGONO NCHINI


Baadhi ya watu waliojitokeza kwenye maadhimisho ya ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yenye lengo kujadili kampeni ya kutokomeza rushwa ya ngono nchini.

Na Mussa Khalid Dar es salaam

Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja katika kuvidhibiti vitendo vya ukatili wa kijinsia wanaokumbana nao wanawake ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa ya wahusika wanapowabaini.

Wito huo umetolewa leo Novemba 27,2019 jijini Dar es salaam na wadau kutoka taasisi mbalimbali za wanawake katika maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yenye lengo kujadili kampeni ya kutokomeza rushwa ya ngono nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi wa wanawake Tanzania Marry Rusimbi alisema kutokana na ukatili wa ngono kutoongelewa kila wakati imepelekea waanzishe kampeni ya kukomesha vitendo hivyo.

Aidha alisema wanakampeni ya muunganiko wa ushirika na wanaharakati mbalimbali uitwao mtandao wa kupinga rushwa ya ngono Tanzania.

Awali akizungumza Mwenyekiti kamati ya wanawake  Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania Rehema Ludanga aliwata wafanyakazi wanaofanyiwa ukatili wa kingono kujitokeza kutoa taarifa ili wasaidiwe kwa wakati.

“Baada ya kuwa tumesema kwa muda watu wameanza kujtokeza hivyo naendelea kusisitiza waendelee kujitokeza ili kutoa taarifa zitakazofanya kupata tawimu ya pamoja “alisema Rehema

“Zamani watu wengi walikuwa wanaona ni siri jambo hilo kwani mpaka sasa kwa takwimu za nchi zinaonyesha ni asilimia 28 ya wanawake wananyanyasika kijinsia kwa mwaka nasi wafanyakazi tunaingia katika gurudumu hili la nchi nzima”aliendelea kusisitiza Rehema

Agnes Lukanda kutoka Binti Leo Mtandao wa wasanii wanawake Tanzania alisema ni vyema jamii ikaunga mfumo wa pamoja katika kupambana na vitendo vya rushwa ya ngono.

“Mini ninacho kishauri ni kwamba tuangalie ni kwa vipi tunaweka mifumo ya wazi ya utoaji huduma zilizobora  itakayomfanya mwanamke asikamatwe na rushwa ya ngono”alisema Lukanda

Maadhimisho hayo yaliambatana na kauli mbiu isemayo  “kataa rushwa ya ngono jenga kizazi chenye usawa”yamehudhuriwa na maafisa wa TAKUKURU,Tanzania Polisi,TAWAJA,WAJIKI ili kujadili ujenzi wa nguvu ya pamoja katika kuendeleza vita dhidi ya Rushwa ya ngono.


No comments