NEEMA ZANZIBAR, SMZ YAPATA GAWIO LA BILIONI 25
Rais wa
Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein
Na
Iddi Haji, Maelezo, Zanzibar
Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar imepatafaida zaidi ya shilingi bilioni 25 ikiwa ni malipo ya huduma za matumizi ya
mkonga wataifa, SerikalimtandaoVisiwani Zanzibar
Mkurugenzi
Mtendaji Wakala wa Mkonga wa Mawasiliano Zanzibar, Mhandisi Shukuru Awadhi
Suleiman amesema kwamba fedha hizo zimelipwa kutoka katika makapuni ambayo yanatumia
huduma zao.
“TumepatafedhahizoambazokutokaKampuniyasimuya
ZANTEL ikiwanimalipokuanziamwaka 2013 hadimwaka 2024” AlisemaMkurugenzihuyo.
Alisema
kwamba Serikali mtandao imekuwa nafaida kubwa kwa wananchi ambapo sasa huduma zaa
fya, kodi na elimu zimekuwa zikitolewa kwa urahisi na ufanisi mkubwa.
Amesema
katika sekta ya afya, kumekuwa na mafanikio makubwa katika huduma, vituo vya afya
24 Unguja na Pemba vimeunganishwa katika mfumo wa Serikali mtandao.
“Leo
hii mgonjwa anaweza kufanyiwa vipimo kama vya X-ray katika hospitali ya Kivunge
Mkoa Kaskazini Unguja na, vipimo vile vitasomwa Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja
bila ya mgonjwa au daktari kulazimika kusafiri” Alisema Mkurugenzi Mhandisi Shukuru.
Mkurugenzi
huyo amesema kwa kutumia huduma za Serikali Mtandao, huduma za vyeti vya kuzaliwa
imekuwa rahisi kwa sasa kwani wananchi wanapata vyeti vya kuzaliwa katikaWilaya
zao.
“Sasa
hivi Wakala wa Usajili na Matukio ya Kijamii Zanzibar wanatumia huduma hizi, watu wanapata vyeti vyao
vya kuzaliwa katika Wilaya zao, wanaomba huko na taarifa zao zinatumwa Makao Makuu
na kufanyiwakazi” Alisema Mkurugenzi Shukuru.
Mbali
ya sekta hizo, pia Kampuni ya Uunganganishaji Maudhui ya ZMUX inatumia mkonga wataifa katika kurusha matangazo
ya Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).
Akizungumziasektayakodi,Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema kwamba Bodi ya Mapato Zanzibar
nimoja yawatumiaji wakubwa wahuduma za Serikali mtandao ambapo sasa huduma za kodi zimeunganishwa katika mtandao mmoja.
Mwisho.
No comments