WAZIRI BITEKO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI BUKOMBE
Waziri wa Madini Doto Biteko,
Tito
Mselem Bukome,
Waziri wa Madini Doto Biteko, amekagua miradi ya
maendeleo katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita na kuwataka madiwani wilayai
humo kutoa ushirikiano kwa watalamu ili kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.
Waziri Biteko alitoa wito huo wakati alipotembelea
miradi ya ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondari Iguwa na shule ya msingi
Mwalo zilizopo wilayani Bukombe.
Katika kutekeleza hayo Waziri Biteko alichangia
vifaa vya ujenzi kwenye shule ya msingi Segwe, Mwalo pamoja na shule ya
Sekondari ya Iguwa zilizopo wilayani humo ili kuharakisha ukamilishwaji wa
shule hizo.
Waziri Biteko, alitoa mifuko 250 ya saruji katika
shule ya msingi Segwe huku shule ya msingi Mwalo alitowa mifuko ya saruji 123
pamoja na kuchangia matofali zaidi ya 2500 katika shule ya sekondari Igewa ili
kukamilisha ujenzi wa madarasa katika shule hizo.
Pamoja na mambo mengine, Waziri Biteko aliwataka Viongozi
wa Kisiasa kusimamia miradi ya maendeleo kikamilifu na kuhakikisha wakati wa
kampeni haukwamishi miradi kuendelea kujengwa, hayo aliyabainisha baada ya
Diwani wa kata ya Igulwa Richadi Mabenga kudai kuwa wakati wa uchaguzi wa
serikali za mitaa ujenzi ulisimama ili watu waingie kwenye michakato ya
kisiasa.
Awali mkuu wa shule ya msingi Segwe Simon Sombi,
alisema shule hiyo inawanafunzi 452 wasichana 227 wavulana 225 na kwamba
wanafunzi wa darasa la pili walikuwa wanasomea chini ya miti kabla ya darasa la
saba kuhitimu kutokana na upungufu wa madarasa.
Sombi alimushukuru Waziri Biteko kwa kuchangia
hali ambayo itapunguza uhaba wa madarasa ingawa kunachangamoto zingine za
upungufu wa nyumba za walimu.
Pia, Mkuu wa shule ya msingi Mwalo Makoye Ludubala,
alishukuru mchango wa Waziri Biteko na kumhakikishia ufaulu mkubwa kwa
wanafunzi katika shule hiyo.
“Shule ya Msingi Mwalo ina jumla ya wanafunzi 361
ikiwa wavulana 187 wasichana 174 na muhimu zaidi shule yetu imeshika nafasi ya kwanza
kimkoa na ninakuahidi kuendelea kufanya vizuri katika mitihani ya kitaifa,”
alisema Ludubala.
Kwa upande wake Muhandisi wa ujenzi wilaya ya
Bukombe Dominico Shilingo aliunga mkono juhudi za Waziri Biteko na kuongeza
kuwa hapa hakuna sababu ya kuchelewa kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa vyumba
nane vya madarasa katika shule ya sekondari ya Iguwa iwapo Diwani wa eneo hilo
atatoa ushirikiano kwa watalamu na kuhamasisha wananchi kujitolea nguvu zao.
Muhandisi Shilingo alisema changamoto ya wataalamu
kukosa ushirikiano kwa madiwani na wenyeviti wa mitaa ni kikwazo kikubwa kwenye
maendeleo ya miradi hapa nchini.
Nae, Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya
Bukombe Dioniz Myinga aliomba wananchi kuendelea kushiriki kwenye miradi ya
maendeleo kwa kujitolea nguvu zao kwa kusomba kokoto, maji na mchanga ili
kumuunga mkono Waziri wa Madini ambae ndiyo Mbunge wa Jimbo la Bukombe.
Mabenga alisema walifikia hatuwa ya kusimama
kupisha uchaguzi wa serikali za mitaa na kwamba uchaguzi umeisha watahakikisha
mradi unakamilika ifikapo Januari 2020 ili wanafunzi wa kidato cha kwanza
waanze kutumia madarasa hayo.
No comments